JICHO KWA JICHO!
MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Banana Zorro jana usiku alipanda jukwaa la Mashauzi Classic ndani ya ukumbi wa Mango Garden na kupiga bonge la ‘kolabo’ na Isha Mashauzi.
Kwa pamoja wasanii hao walitambulisha rasmi jukwaani wimbo wao waliouimba pamoja unaokwenda kwa jina “Ukinipenda” ambao ndani yake Isha ametambaa katika miondoko ya Ki-bongo fleva.
Wimbo huo ambao utakuwepo kwenye albam ya Isha Mashauzi ya miondoko ya Bongo Fleva, ulifanikiwa kuuteka ukumbi wa Mango Garden.Chanzo:www.saluti5.com
Advertisements