Month / December 2012
UKURASA WA MBELE GAZETI LA MWANANCHI
Lissu asema Profesa Shivji amepotoka kuponda kesi ya Lema
Fredy Azzah
HATUA ya mwanazuoni wa siku nyingi nchini, Profesa Issa Shivji kupinga hukumu ya Mahakama ya Rufani Tanzania iliyomrejeshea ubunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema imemtia matatani na baadhi ya watu wanasema gwiji huyo wa sheria “huenda amenukuliwa vibaya au hajasoma hukumu husika.”
Jana Wakili wa Lema, Tundu Lissu, alimkosoa Profesa Shivji pamoja na Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika, Francis Stolla akisema wanasheria hao wamepotoka katika matamshi yao ya kupinga hukumu ya Mahakama ya Rufani.
UKURASA WA MBELE GAZETI LA MWANANCHI
TAMKO RASMI LA BAVICHA MKOA WA TANGA KUHUSU KATIBU WA BAVICHA MKOANI WA TANGA BW DEOGRATIAS KISANDU
katiba ya CHADEMA hasa katika Sura ya 10 inayozungumzia Maadili ya Viongozi, Sifa mahususi za viongozi na maadili ya wanachama, kifungu
10.1(1-13), toleo la mwaka 2006.
UKURASA WA MBELE GAZETI LA MWANANCHI
Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi (UBT) kuhama januari 2013
Akizungumzana wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Jiji Mussa Zungiza, alisema lengo la kuhamisha kituo hicho ni kwa ajili ya kupisha Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DART).
Zungiza alisema uhamishaji kabisa wa kituo hicho cha Ubungo kutategemea kukamilika kwa ujenzi wa kituo hicho kipya cha Mbezi. Chanzo:fullshangweblog
UKURASA WA MBELE GAZETI LA TANZANIA DAIMA
TAARIFA KWA UMMA JUU YA MAAMUZI YA BARAZA LA MADAKTARI KUHUSU MADAKTARI WALIOGOMA
Baraza lilipitia malalamiko yote na limetoa adhabu stahiki kwa kila daktari aliyethibitishwa kushiriki katika mgomo huo. Adhabu hizo zilikuwa katika makundi yafuatayo; onyo, onyo kali na kusimamishwa udaktari kwa muda wa kati ya mwezi mmoja na miezi sita.Vile vile kuna Madaktari ambao hawakuwa na hatia ya kushiriki katika mgomo na hivyo walifutiwa mashtaka.
MCHANGANUO WA ADHABU
- Waliofutiwa mashitaka madaktari 49
- Waliopewa onyo madaktari 223
- Waliopewa onyo kali madaktari 66
- Kusimamishwa kwa muda madaktari 30
- Mashitaka yaliyoahirishwa kutokana na wahusika kuhitaji ushauri wa kisheria madaktari 4
- Mashitaka yasiyosikilizwa kutokana na wahusika kutofika walipoitwa na Baraza madaktari 22
Wizara inakamilisha taratibu za kinidhamu kwa mujibu wa Kanuni za Utumishi wa Umma kwa Madaktari wote waajiriwa ambao walipatikana na hatia mbele ya Baraza la Madaktari. Wizara pia imeridhia kuwapa Madaktari waliokuwa katika mafunzo kwa vitendo fursa nyingine ya kuendelea na mafunzo hayo katika hospitali za Umma walizokuwepo kabla ya kuondolewa. Hata hivyo fursa hii haitawahusu Madaktari wote waliopewa adhabu za kusimamishwa na Baraza la Madaktari, hadi hapo watakapomaliza kutumikia adhabu zao.
HITIMISHO
Kwa taarifa hii madaktari wote waliofutiwa mashtaka na wale waliopewa onyo na onyo kali wanatakiwa kuwasilisha kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii barua kutoka kwa msajili wa Baraza la Madaktari ikithibitisha kurejeshewa usajili na kuruhusiwa kuendelea na mafunzo kwa vitendo. Vile vile madaktari waajiriwa(Registrar) wanatakiwa pia kuripoti kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya ili kupewa barua zao kulingana na Adhabu walizopewa. Barua hizi zitatolewa kuanzia tarehe 2 Januari, 2013.Madaktari wote walio katika mafunzo kwa vitendo wanatakiwa kuanza kazi katika vituo vyao vya awali ifikapo tarehe 14 Januari, 2013.Hakuna muda utakaoongezwa kwa kipindi kilichobakia cha mafunzo kwa vitendo. Kwa wale wote waliopewa adhabu wataanza kutumikia adhabu hizo kuanzia tarehe ya adhabu hiyo ilivyotolewa.
Nsachris Mwamwaja
Msemaji
WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
27/12/2012
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Singida alumbana na diwani wa viti maalum (CCM) kuhusiana na ripoti ya Sikika.
Dk.Henry Mmbando,wa ofisi ya mganga mkuu wa halmashauri ya wilaya ya Singida akitoa ufafanuzi juu ya tuhuma zilizotolewa na shirika la Sikika juu ya uwajibikaji katika kutoa huduma katika halmashauri hiyo.(Picha na Nathaniel Limu).
Mwanakamati wa shirika lisilo la kiserikali la Sikika, diwani (CCM) Salima Kundya akimtuhumu diwani wa mkutano huo diwani Elia Digha (hayupo pichani) kwa kauli yake kuwa kamati ya Sikika haijui kitu chochote kuhusu na utoaji wa huduma ya afya katika halmashauri ya wilaya ya Singida. Salima alikuwa akitoa tuhuma hizo mbele ya mkutano wa mrejesho wa taarifa ya uwajibikaji katika utoaji wa huduma za afya iliyokuwa ikitolewa na shirika la Sikika.
Na Nathaniel Limu.
Halmashauri ya wilaya ya Singida imesema haitakubali kuchonganishwa na wananchi wake na vyombo au taasisi yakiwemo mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs), kwa kutoa taarifa zisizofanyiwa utafiti wa kina.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Alli Juma, amesema hayo muda mfupi kabla ya mkutano wa mrejesho wa ripoti/taarifa ya shirika lisilo la kiserikali la Sikika lenye makazi yake jijini Dar-es-salaam, iliyohusu ufuatiliaji wa uwajibikaji katika utoaji wa huduma za afya, haujafungwa rasmi.
Amesema taarifa iliyotolewa na shirika la Sikika, kwa kiasi kikubwa haikufanyiwa utafiti wa kina, kitendo ambacho kinaweza kusababisha halmashauri kutokuelewana vizuri na wananchi wake.
Alli ambaye ni Afisa Utumishi amesema Sikika hawakuwa na mawasiliano wala ushirikiano mzuri na wakuu wa idara katika kupata ukweli wa taarifa mbalimbali walizokuwa wanazikusanya.
“Mimi niwaombeni tu ndugu zangu wa Sikika, fanyeni kazi kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu, halafu mkiandika mabaya, upande wa pili andikeni pia mazuri hata kama yapo machahe”,alisema Alli.
Mkutano huo uliokuwa chini ya uenyekiti wa diwani (CCM) Elia Digha, Mwenyekiti huyo alitoa shutuma nzito kwamba wafanyakazi wa Sikika na kamati nzima iliyofuatilia uwajibikaji wa huduma za afya, haijui lolote.
“Mimi nasema timu yote iliyoleta taarifa hii, haijui lolote, naomba siku za usoni tushirikiane vizuri katika kufuatilia uwajibikaji katika sekta zote, kutoa taarifa za jumla jumla kama hii, mtaacha watu waichukie bure serikali”, alisema Digha ambaye ni diwani wa kata ya Msange jimbo la Singida Kaskazini.
Baada ya maneno hayo mazito, diwani wa viti maalum (CCM) Salima Kundya, aliyeshiriki na Sikika kufuatilia uwajibikaji katika sekta ya afya, alimtolea uvivu Mwenyekiti Digha, kuwa lengo lake ni kutaka kuficha ukweli uliopo kwenye taarifa hiyo.
“Kama sisi madiwani wawili wa CCM mliotuchagua tukashirikiane na Sikika na tukabaini yote yaliyopo kwenye taarifa ya Sikika kuwa ni ya ukweli mtupu, halafu wewe unasema hatujui lo lote, basi wewe mwenyekiti Digha na madiwani wote wa CCM walioshiriki kutachagua na ninyi wote hamjui kitu au cho chote kinachofanyika ndani ya halmashauri hii”, alisema Salima huku uso wake ukionyesha kujawa na hasira.
Baada ya maneno hayo ya diwani Salima, bila kulazimishwa, Digha ambaye pia ni msaidizi wa mbunge wa jimbo la Singida kaskazini Lazaro Nyalandu, alisimama na kuomba radhi kwa matamshi yake ambayo yalilenga kuidhalilisha kamati iliyoambatana na Sikika.
Katika mengi yaliyomo kwenye taarifa ya Sikika, kuna hoja iliyotolewa na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali, inaonyesha kuwa halmashauri hiyo ilikuwa na shilingi bilioni 1,686,561,960 za miradi mbalimbali ya maendeleo.
Lakini taarifa hiyo, ilionyesha kiasi cha shilingi bilioni 1.6 sawa na aslimia 61.4,hazikutumika kwa wakati, kitendo hicho kinamaanisha kuwa baadhi ya miradi ya maendeleo, ilikamilika nusu ama haijakamilika kabisa.chanzo:moeblog