Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ampa pole Chief wa Wahehe , Adam Abdu Sapi Mkwakwa


1

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Chief wa Wahehe , Adam Abdu Sapi Mkwakwa   wakati alipokwenda nyumbani kwa Chief huyo, Kalenga Iringa  Februari 20, 2015 baba yake Chief huyo, Marehemu Abdu Adam Sapi Mkwawa uliotokea hivi karibuni.

(Picha zote na Ofisi ya Waziri Mkuu)

2

  Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akishiriki katika dua mbele ya kaburi la marehemu Abdu Adam Sapi Mkwawa   wakati alipokwenda nyumbani kwa Chief huyo, Kalenga Iringa   kuhani.

6

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizunbgumza na viongozi wa wilaya ya Kilolo baada ya kusomewa taarifa ya wilaya hiyo Februari 21, 2015. Kushoto ni Mkuu wa koa wa Iringa, Amina Masenza.

7

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  na mkewe Tunu  wakisalimiana na walimu  wa sekondari ya Ilula kabla ya kukagua ujenzi wa maabara katika shule hiyo akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa.

8

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua moja ya madara ambayo yamegeuzwa kuwa maabara katika Shule ya Sekondari ya Ilula akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa Februari 21, 2015. Kitendo hicho hakikumfurahisha na aliagiza kisirudiwe tena sehemu nyingine ngo mapya yajengwe kwa ajili ya maabara

9

Mke wa Waziri Mkiuu, Mama Tunu Pinda akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Ilulawilayani Kilolo ambako Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alikagua ujernzi  wa maabara na kuhutubia wananchi. 

10

Mkuu, Mizengo Pinda akikagua banio katika mradi wa umwagiliaji maji wa kijiji cha  Nyanzwawilayani Kilolo akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa Februari 21, 2015.

12

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Tunu wakikagua shmba la vitunguu la Bw. Furaha Ngalali  (kulia)  wakati walipotembelea mradi wa umwagiliaji wa kijiji cha Nyanzwa wilayani  Kilolo Februari 21, 2015.

13

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na   Meneja Mipango wa Kamouni ya Mawasiliano ya simu ya VIETTEL TANZANIA LIMITED tawi la Iringa, Salvatory Elikidus katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri Mkiuu, Mizengo Pinda katika kijiji Nyanzwa wilayani Kilolo Februari 21, 20154.  Kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Tawi la Iringa,  Tran  Nhat Duy na wapili kushoto ni  Mkuu wa Idara ya Fedha, Vo Ngoc Thang.

Rais wa Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein afungua Madrasatul Al-Tawheed wilaya ya kusini unguja


unnamed

Rais wa Zanzibar na Mwenmyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akifungua pazia kuifungua  Madrasatul Al-Tawheed iliyopo Kiongoni Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja jana alipofanya ziara maalum katika wilaya hiyo (kushoto) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi na Utumishi wa Umma Mhe,Haroun Ali Suleiman,

[Picha na Ikulu.]

THE MOHAMED AMIN AFRICA MEDIA AWARDS – CALL FOR ENTRIES


MAAMAS_MOSOUND_LOGO-2

Mohamed Amin Africa Media Awards – Celebrating Excellence

AFRICA24 MEDIA, the Pan African, international quality, multi-platform content provider, joins MoSound, East Africa’s premiere events company, to debut our new awards program that will honor the best quality, most innovative content, and rising platforms that are changing the face of Africa.

May 20-22 in Nairobi, Kenya we are inviting the continent’s media to learn at 6 daily workshops; discuss, at 3 daily symposiums; and win at our gala dinner. Today we start accepting nominations from both content makers, and their fans, on our awards website, www.mohamedaminama.com.

Awards will be given in the following categories:

BEST NEWSCAST

BEST SPORTS CONTENT

BEST USE OF VISUAL CONTENT IN SOCIAL MEDIA

BEST MAGAZINE PROGRAM

BEST CSR INITIATIVE PRESENTATION

BEST MOBILE PHONE CONTENT FEATURING AFRICAN IMAGES MOST INNOVATIVE PROGRAM

BEST DOCUMENTARY

STUDENT AWARD: I AM AFRICA

MAAMA’S BEHIND THE SCENES AWARD

PEOPLE’S CHOICE AWARD (VOTED AMONG ALL CATEGORIES)

Detailed descriptions and criteria for each award are available on the website. Workshops will feature expert instruction from international media professionals on Sports Event Coverage; News Writing; Effective Use of Social Media; Camerawork Innovation; Line Producing Newscasts; and Presenting on Talk Shows. Symposiums will line up prominent featured speakers to discuss Television Production Standards; Reporting on Crises/Disasters/Political Conflict in Africa; Media Freedom/Responsibility.

All categories are open to content in any language spoken in Africa, and encouraged from media organizations LARGE and small. Awards will include paid contracts to produce content for current and future AFRICA24 MEDIA productions.

A panel of respected judges will be announced in March, as well as our exciting venues and daily excursions to see some of the top tourists spots in Nairobi.

Enter your productions or those you admire today, and you could wind up a finalist, with an all expense paid trip to Nairobi to participate in the 3-day event and be honored at the gala dinner.

The event has been officially announced from Chester House in Nairobi, where the renowned photographer and video journalist Mohamed Amin kept his office until his death in a plane crash in 1996. The Camerapix/ AFRICA24 MEDIA founder was passionate about quality television and trained many young Africans who found venerable careers in media here. His reports of the mid-80’s Ethiopian famine led to relief efforts that saved millions. His coverage of the rise and fall of Idi Amin, the assassination of Tom Mboya, the Soviet training base in Zanzibar and the coronation of Bokassa as Emperor of the Central African Republic, go down in journalistic lore. But he also favored Africa with dozens of coffee table books, beautiful travelogues and annual coverage of the East African Safari rally.

If my Dad was alive today, his son Salim says, “he would surely embrace every form of media, to reach people, to tell new stories, and to drive his business.”

He would also be proud that an event named after him would provide training and important dialogue about his profession. And he would be impressed that AFRICA24 MEDIA is offering prizes that include contracts to produce content for his company.

Africa’s current generation of TV professionals, as well as those about to launch their careers, can be proud to participate in categories honoring innovative programs, social media and, of course, the student award!

A video press release is also available at www.mohamedaminama.com

TAMKO LA UVCCM MKOA WA LINDI LA KULAANI MAUAJI YA ALBINO NA KUMPONGEZA RAIS JAKAYA KIKWETE KWA UTEUZI WA WAKUU WA WILAYA


Baraza Kuu la Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Lindi chini ya Mwenyekiti wake Ndugu Amir M. Mkalipa, wamefanya kikao cha kikanuni leo tarehe 21 feb 2018, katika ukumbi wa mikutano wa ofisi kuu ya CCM Mkoa wa Lindi, iliyopo Wailes, Lindi mjini.
Pamoja na kujadili hoja zingine zinazohusu uimara wa jumuiya mkoani Lindi, changamoto za Vijana na Walimu, suala la migomo ya wafanyabiashara, na kuwataka watendaji wa Serikali kutimiza wajibu na majukumu yao kikamilifu ili kuongeza ufanisi wa Serikali katika kutatua kero za wananchi na kuleta maendeleo ya jamii, lakini pia kikao hicho kimeazimia:-
a} Baraza kuu la UVCCM Mkoa wa Lindi imeitaka Serikali kuendelea kuchukua hatua kali kwa watakaobainika kuhusika na mauaji ya Albino. Ni lazima Serikali kushirikiana na wananchi wahakikishe ndugu zetu Albino wanaishi maisha yenye usalama, amani na furaha kwani ni haki yao kikatiba.
b}Pia, Baraza Kuu la UVCCM Mkoa wa Lindi linampongeza Mhe. Rais na Mwenyekiti wa CCM ndugu Jakaya Kikwete kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM (2010-2015) kwa kukamilisha ujenzi wa barabara ya Kibiti-Mingoyo,
Pia inampongeza Mhe Rais Jakaya Kikwete kwa kuteuliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa jumuiya ya Afrika Mashariki.
Lakini pia, UVCCM inampongeza na kumuunga mkono Mhe Rais kwa uteuzi wa wakuu wa wilaya wapya 27 ambapo baadhi ya wateule hao wanatoka kwenye jumuiya hiyo, jambo ambalo ni heshima kubwa kwa UVCCM, na kudhihirisha kuwa jumuiya hiyo inatimiza wajibu wake wa kuwa tanuru la kuoka viongozi wenye uwezo, waadilifu na wenye kuaminika katika jamii. Pia UVCCM imewapongeza ndugu Mboni Mhita na ndugu Paul Makonda kwa kuteuliwa kuwa wakuu wa wilaya na kuwataka wakatimize wajibu kwa kuwatumikia wananchi kwa uadilifu na ufanisi.
Pia, UVCCM Lindi inampongeza Kamanda wa Vijana Mkoa Mhe Bernard Membe-Mbunge wa Mtama na Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa kwa kuwa karibu na Vijana na kuiwezesha jumuiya kutimiza majukumu yake.
C} Mwisho, UVCCM Mkoa wa Lindi inahimiza Halmashauri za wilaya kutenga asilimia 10% ya Mapato yake kwa ajili ya maendeleo ya Vijana na Wanawake, ili vijana wanufaike kwa mikopo na waweze kujiajiri ili kukabiliana na tatizo la ajira na umasikini. Jambo hili lipo kisheria sio ombi, hivyo watendaji husika wa Serikali wahakikishe wanatimiza wajibu wao ipasavyo ama UVCCM itawalazimisha kutimiza wajibu huo.
Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Lindi, wamepitisha ratiba ya shughuli zao kwa Mwaka 2015 na wataanza ziara ya kutembelea Vijana katika wilaya zote sita (6) za Mkoa wa Lindi.

Imetolewa na:-

 

……………………….

SAID Y. GOHA

KATIBU WA UVCCM MKOA, LINDI

Mchango Mbunge wa Kigoma Kaskazini -Chadema na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Hesabu za Mashirika ya Umma Zitto Kabwe Kuhusu Tozo za Mahoteli yaliyomo Hifadhini


Mbunge wa Kigoma Kaskazini -Chadema na Mwenyekiti  wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Hesabu za Mashirika ya Umma Zitto Kabwe
 Kilimo

Mheshimiwa Spika,

Mwaka 2014 umekuwa ni mwaka mwema kwa sekta ya kilimo nchini. Uzalishaji umeongezeka, mazao ya chakula tumezalisha ziada kwa 125% ya mahitaji yetu ya chakula. Kwa upande wa mazao ya biashara, zao la Korosho limeweka rekodi Mpya kwa kuzalisha takribani tani 200,000 za Korosho.

Hata hivyo wananchi hawana furaha na mafanikio haya kwa sababu ya kutojiandaa kwetu. Wakulima wa mahindi hawajalipwa na bado tunahangaika na soko la mahindi na mchele. Serikali bado inaruhusu Mchele kutoka nje kuingia nchini ilihali mchele wetu unakosa soko. Maghala ya kuhifadhi nafaka bado kujengwa na Serikali inasema inaongea na nchi ya Poland kupata mkopo wa kujenga maghala. Ni kama vile Serikali haikuwa na mipango wakati inajua kuwa uzalishaji utaongezeka zaidi ya maradufu.

Taarifa ya UTEUZI Kutoka IKULU:Rais Jakaya Kikwete Amteua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dkt. Hamisi Hassan Mwinyimvua (pichani) kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, anayesimamia Menejimenti ya Fedha za Umma (Public Finance Management). Kabla ya uteuzi wake, Dkt. Mwinyimvua alikuwa Msaidizi wa Rais wa muda mrefu wa masuala ya uchumi. Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Yohana Sefue leo, Jumatatu, Februari 2, 2015, imesema kuwa uteuzi wa Dkt. Mwinyimvua ulianza Jumamosi, Januari 24, 2015. Dkt. Hamisi Hassan Mwinyimvua ni mwanataaluma mwenye ujuzi na uzoefu mkubwa katika uchumi. Anayo shahada ya kwanza ya B.A. (Econ) ya Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (1986), Shahada ya Uzamili ya M.A. (Econ) ya Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (1988) na Shahada ya Uzamivu ya PhD ya uchumi kutoka vyuo vikuu vya Dar es Salaam na Lund cha Sweden. Dkt. Mwinyimvua amekuwa mhadhiri wa miaka mingi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambako amepanda daraja kutoka Tutorial Assistant, mwaka 1986-1988, Mhadhiri Msaidizi, mwaka 1988-1996, Mhadhiri, mwaka 1996-2005, Mhadhiri Mwandamizi, mwaka 2005-2006 na Mkuu wa Idara ya Uchumi ya chuo hicho mwaka 2006. Dkt. Mwinyimvua aliteuliwa kuwa Msaidizi wa Rais, Uchumi, mwaka 2006, nafasi ambayo ameishikilia hadi mwaka huu, 2015. Imetolewa na: Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, DAR ES SALAAM.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dkt. Hamisi Hassan Mwinyimvua(pichani) kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, anayesimamia Menejimenti ya Fedha za Umma (Public Finance Management).

Kabla ya uteuzi wake, Dkt. Mwinyimvua alikuwa Msaidizi wa Rais wa muda mrefu wa masuala ya uchumi.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Yohana Sefue leo, Jumatatu, Februari 2, 2015, imesema kuwa uteuzi wa Dkt. Mwinyimvua ulianza Jumamosi, Januari 24, 2015.

Dkt. Hamisi Hassan Mwinyimvua ni mwanataaluma mwenye ujuzi na uzoefu mkubwa katika uchumi.

Anayo shahada ya kwanza ya B.A. (Econ) ya Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (1986), Shahada ya Uzamili ya M.A. (Econ) ya Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (1988) na Shahada ya Uzamivu ya PhD ya uchumi kutoka vyuo vikuu vya Dar es Salaam na Lund cha Sweden.

Dkt. Mwinyimvua amekuwa mhadhiri wa miaka mingi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambako amepanda daraja kutoka Tutorial Assistant, mwaka 1986-1988, Mhadhiri Msaidizi, mwaka 1988-1996, Mhadhiri, mwaka 1996-2005, Mhadhiri Mwandamizi, mwaka 2005-2006 na Mkuu wa Idara ya Uchumi ya chuo hicho mwaka 2006.

Dkt. Mwinyimvua aliteuliwa kuwa Msaidizi wa Rais, Uchumi, mwaka 2006, nafasi ambayo ameishikilia hadi mwaka huu, 2015.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

SERIKALI YAJENGA BARABARA ZENYE UREFU WA KILOMETA 42 MJI WA DODOMA


jeni

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama akijibu swali Mbunge Bungeni.

Na Lorietha Laurence-Maelezo , Dodoma
SERIKALI kupitia mradi wa uendelezaji miji (TSCP) imefanikiwa kujenga barabara zenye urefu wa kilometa 42 kwa mji wa Dodoma kwa msaada wa mfuko wa Benki ya Dunia.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama ameeleza hayo Bungeni Dodoma, kuwa ujenzi huo wa barabara umehusisha pia ujenzi wa mifumo ya maji ya mvua ,dampo la kisasa kwa kijiji cha Chidaya pamoja na mitambo y usombaji taka.

Read more…