Month / September 2014
SITTA APOKEA MESEJI ZA MATUSI
Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samuel Sitta amesema anapokea meseji za simu zaidi ya 50 kwa siku za kumtukana na kusisitiza ataendelea kupambana kuhakikisha Katiba inayopendekezwa inapatikana.
Sitta alitoa kauli hiyo bungeni mjini Dodoma jana wakati akielezea kutoridhishwa kwake na kile alichodai ni namna hukumu ya kesi iliyofunguliwa na Saed Kubenea inavyopotoshwa na wanaomchukia.
“Kuna baadhi ya vyombo vya habari wananichukia mimi binafsi. Wasichanganye chuki hizo na mchakato wa Bunge Maalumu,” alisema Sitta na kuongeza;
“Mimi napokea matusi kila siku. Meseji zisizopungua 50 viongozi wa Chadema wameweka namba zangu katika tovuti nitukanwe kila siku hilo mimi niko tayari na mnaniona niko safi tu wala sihangaiki nalo.”
“Lakini sasa Bunge Maalumu ni chombo cha kikatiba, kiko tofauti na mwenyekiti wake. Huwezi kuliadhibu Bunge Maalumu kwa sababu hupendi sura ya mwenyekiti wake,” alisema.(P.T)
BUNGE MAALUM LA KATIBA LAPENDEKEZA MAKAMU WA TATU WA RAIS
Na Mwandishi wetu_MAELEZO_Dodoma
Bunge Maalum la Katiba limependekeza muundo wa uongozi wa Serikali utakuwa na Makamu watatu wa Rais wa Jamhuri Muungano wa Tanzania.
Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Uandishi wa Bunge Maalum la Katiba,Mhe. Andrew Chenge wakati akiwasilisha Rasimu ya Katiba inayopendekezwa wakati wa kikao cha arobaini na mbili cha Bunge hilo.
Amesema kuwa katika mapendekezo hayo mgombea mwenza ndio atabaki kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais, na kwa upande wa Rais wa Zanzibar atakuwa Makamu wa Pili na Waziri Mkuu atakuwa Makamu wa tatu wa Rais.(P.T)
MKATABA WA MOSOTI, SIMBA UMEVUNJWA – FIFA
Mshambuliaji wa Timu ya Yanga, Mrisho Ngassa (17), akimpiga chenga aliyekuwa beki wa Simba, Mkenya, Donald Mtosi wakati mchezo wao wa Nani Mtani Jembe mwezi Desemba mwaka jana
Na Bertha Lumala, Dar es Salaam
Wakati uongozi wa Simba ukidai kuwa bado una mkataba na beki Mkenya Donald Mosoti, Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) limeitaka klabu hiyo kumlipa fidia beki kwa kuwa mkataba wake umevunjwa.
Katibu Mkuu wa Simba, Stephen Ally alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini jana akisema kuwa Mosoti bado ni mchezaji wao halali kwa vile mkataba kati yao na mchezaji huyo badi haujavunjwa.
Donaldi Mosoti akiwa kazini enzi zake Simba sc
Klabu hiyo kongwe nchini, iliamua kumwacha beki huyo dakika za mwisho za usajili msimu huu ili kumsajili Emmanuel Okwi aliyevunja mkataba wake na Yanga huku mwanasheria wa Mosoti, Felix Majani akidai kuwa uamuzi huo ulifanywa bila kumshirikisha mteja wake.(P.T)
LIVERPOOL YABANWA 2-2, YATOKEA KWENYE PENALTI 14-13 ANFIELD
Mario Balotelli akipambana jana Anfield
KLABU ya Liverpool imeifunga Middlesbrough kwa penalti 14-13 katika Raundi ya Tatu ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 120 Uwanja wa Anfield.
Kinda Jordan Rossiter alianza kuwafungia Wekundu hao baada ya kupewa nafasi ya kwanza kuchezea kikosi cha kwanza, kabla ya Adam Reach kuwasawazishia wageni akimalizia pasi ya Grant Leadbitter.
Mchezo huo ulihamia kwenye muda wa nyongeza kufuatia timu kumaliza zikiwa zimefungana 1-1 baada ya dakika 90.(P.T)
Kikwete addresses UN General Assembly on Tuesday
President Jakaya Kikwete on Monday started a series of meetings that will take a week at the UN General Assembly and other bilateral sessions here in New York.
Wajumbe wa Z’bar watishwa
Dodoma. Hali imeanza kuwa tete Bunge la Katiba kutokana na ujumbe unaosambazwa kwa kasi katika mitandao ya kijamii, ili kuwagombanisha na kuwafitinisha wajumbe wa kundi la 201 kutoka Zanzibar.
Ujumbe huo ambao gazeti hili limeuona, ulianza kusambazwa juzi, ukiwataka wajumbe wa kundi la 201 kutoka Zanzibar, kuondoka bungeni ili theluthi mbili ya Katiba inayopendekezwa isipatikane.
Ban ataka kukomeshwa mashambulizi ya Daesh Syria
Balozi Sefue afunguka Katiba Mpya
Na Elias Msuya, Mwananchi
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue amesema hakuna uwezekano wa kubadili muundo wa muungano kutoka Serikali mbili kwenda Serikali tatu katika mchakato wa Katiba.
Kauli ya Balozi Sefue imekuja ikiwa ni siku chache tangu Rais Jakaya Kikwete kukutana na viongozi wa Kituo cha Demokrasia (TCD) na kutoa uamuzi wa kuahirisha mchakato wa Katiba hadi baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Uhuru Kenyatta atakiwa mahakamani ICC 8,Octoba
Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta atakiwa ICC tarehe 8 OctobaREUTERS/Noor Khamis |