NIC BANK YATOA FEDHA KWA HOSPITAL YA CCBRT


Mkurugenzi wa Banki ya NIC Tanzania  James Muchiri ,akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa hafla ya kukabidhi hundi ya Shilingi milioni Mbili na laki nne 2.4 kwa hospitali ya CCBRT kwa ajili ya wagonjwa wenye, matatizo ya ulemavu katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kushoto ni Mkurugenzi wa Hospitali ya CCBRT Erwin Telemans…
Mkurugenzi wa Hospitali ya CCBRT Erwin Telemans akitoa neno la shukurani kwa uongozi wa Benki ya NIC Tanzania baada ya kukabidhiwa hundi  ya shilingi Milioni 2.4 kwa  ajili ya wagonjwa wenye, matatizo ya ulemavu katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Benki ya NIC Tanzania  James Muchiri…
Mkurugenzi wa Benki ya NIC Tanzania  James Muchiri, akimkabidhi hundi ya shilingi Milioni 2.4 Mkurugenzi wa Hospitali ya CCBRT Erwin Telemans kwa  ajili ya wagonjwa wenye matatizo ya ulemavu katika hafla iliyofanyika  jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Mhe. Zitto Kabwe Atoa Kauli Juu Ya Kufukuzwa Kwa Mheshimiwa David Kafulila NCCR-MAGEUZI


Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe
Leo(Jana)  kwa masikitiko makubwa sana nimesoma kwenye vyombo vya habari kwamba  ndugu David Kafulila kavuliwa uanachama wa chama chake. Kwa hatua hii  David anakuwa amepoteza Ubunge wa jimbo la Kigoma Kusini licha ya kwamba  alichaguliwa na wananchi bila kujali vyama (NCCR-M wanachama wake huko  Kigoma Kusini hawafiki hata asilimia 10 ya wapiga  kura wote). Haya ndio madhara ya Katiba ya sasa. Katakana na historia  ya kisiasa baadhi ya watu wanajaribu kunihusisha na matatizo ya chama  cha NCCR-M. Napenda kuweka wazi kwamba sihusiki kwa namna yeyote ile na  migogoro ya chama kile.
Ninaomba nisihusishwe na mambo yasiyonihusu. Ni  dhahiri kwamba kuvuliwa uanachama kwa David ni jaribio kubwa kwa mfumo  wetu wa demokrasia kama ilivyokuwa huko nyuma wakati kina Erasto Tumbo  walipovuliwa uanachama wa chama chao cha UDP. Ninaamini NCCR-M  watamaliza matatizo yao kwa mujibu wa katiba ya chama chao na ndugu  David Kafulila atazikabili changamoto hizi kama kiongozi kijana wa  kisiasa na kuona hii kama fursa badala ya kukata tamaa. Ifahamike wazi  kabisa kwamba David ni mtu huru mwenye mawazo yake na maamuzi yake.  Kwamba sisi ni marafiki wa karibu na kwamba tunatoka mkoa mmoja haina  maana kwamba lolote afanyalo ama nimemtuma au ninahusika.
Ninaheshimu  misimamo yake na siku zote huwa nipo upande wa anayeonewa, kudhulumiwa  na mnyonge. Msimamo huu wa msingi usiwape watu nafasi ya kunihusisha na  mambo ya chama dhaifu kisicho na dira kama NCCR-M.
Kafulila akumbuke  kwamba hakufukuzwa CHADEMA, alijiondoa mwenyewe. Milango yetu ipo wazi  kwa mujibu wa Katiba, Kanuni na taratibu za chama chetu.
Ndg. Kabwe Zuberi Zitto, Mb
18 Disemba 2011

VODACOM TANZANIA YAZINDUA DUKA JIPYA JIJINI DAR


Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Bw. Jordan Rugimbana akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa duka jipya la kisasa la kampuni ya Vodacom lilipo katika jengo la Quality Center barabara ya Pugu jijini Dar es salaam litakalotoa huduma kwa wateja pamoja na mauzo ya bidhaa mbalimbali za Vodacom. Kushoto ni Meneja Mauzo wa Vodacom Kanda ya Pwani Bw. Henry Tzamburakis.Uzinduzi huo umefanyika mwishoni mwa wiki.. .

Mkuu wa huduma za mauzo ya rejareja wa kampuni ya Vodacom Tanzania Bi. Upendo Richard akimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Bw. Jordan Rugimbana bidhaa mbalimbali zinazopatikana katika duka jipya la mauzo na huduma kwa wateja la kampuni ya Vodacom mara baada ya kulizindua rasmi mwishoni mwa wiki. Duka hilo la kisasa lipo katika jengo la Quality Center, barabara ya Pugu na litatoa huduma za aina zote kwa wateja wa Vodacom…
Mkuu wa Wilaya Kinondoni Jordan Rugimbana akipata maelekezo kutoka kwa Mkuu wa huduma za mauzo ya rejareja wa kampuni ya Vodacom Tanzania Bi. Upendo Richard jinsi ya kutumia Web Box kifaa maalum kinachowezesha matumizi ya kompyuta kupitia televisheni muda mfupi baada ya Mkuu wa Wilaya kuzindua duka jipya la kisasa la Vodacom lililopo katika jengo la Quality Center, barabara ya Pugu jijini Dar es salaam mwishoni mwaka wiki.Kulia ni Meneja Mauzo wa Vodacom Kanda ya Pwani Bw. Henry Tzamburakis.
Mkuu wa huduma za mauzo ya rejareja wa kampuni ya Vodacom Tanzania Bi.  Upendo Richard akimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Bw. Jordan  Rugimbana bidhaa mbalimbali zinazopatikana katika duka jipya la mauzo na  huduma kwa wateja la kampuni ya Vodacom mara baada ya kulizindua rasmi  mwishoni mwa wiki. Duka hilo la kisasa lipo katika jengo la Quality  Center, barabara ya Pugu na litatoa huduma za aina zote kwa wateja wa  Vodacom.
Kampuni  ya Mawasiliano  ya Vodacom Tanzania imezindua duka jipya la kisasa  lililopo katika jengo la kibiashara la Quality Center, kwa ajili ya  kuhudumia wateja wake pamoja na kufanya mauzo likilenga kusogeza karibu  zaidi huduma kwa wateja wake.
Akizindua  duka hilo mwishoni mwa wiki Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan  Rugimbana alisifu juhudi za Vodacom za kutoa huduma bora kwa wateja huku  akiwataka kuongeza ubunifu ili kuwanufaisha watumiaji wa huduma za simu  za mkononi nchini.
“Nimefurahi  kuwa hapa leo kuzindua duka lenu, nawapongeza kwa juhudi zenu za dhati  mnazozifanya katika kutoa huduma bora na namna mnavyowahudumia wateja  wenu na uwepo wa duka hili utapanua wigo wa kuwahudumia kwa uharaka,  urahisi na ukaribu zaidi”Alisema Rugimbana muda mfupi baada ya kufanya  uzinduo huo na kupata fursa ya kutembelea duka hilo lililopo barabara ya  pugu jijini Dar es salaam.
Mkuu  huyo wa Wilaya amesema mpangilio wa duka hilo pamoja na mahali lilipo  ni wazi litatoa faida kubwa kwa jamii na wateja wa Vodacom kampuni  inayoongoza soko la huduma za mawasiliano ya simu za mkononi kwa kuwa na  wateja zaidi ya milioni kumi na moja.
“Kadri  mnavyosogeza huduma zenu karibu na wateja ndivyo hivyo mnavyoongeza  urahisi wa maisha kwa wateja ambao bila ya hivyo watalazimika kusafiri  umbali mrefu kufuata maduka hayo ili waweze kupata huduma ikiwemo  kutatuliwa matatizo wanayokabiliana nayo katika kutumia huduma za  mawasiliano ya simu”Aliongeza Rugimbana huku akitoa rai kwa wananchi  kutumia fursa za maduka hayo kuwa karibu nao kujipatia huduma na  kujifunza.
Awali  akimpatia maelezo Mkuu wa Wilaya. Meneja Mauzo wa kampuni ya Vodacom  Kanda ya Pwani Bw. Henry Tzamburakis alisema kufunguliwa kwa duka hilo  kunalenga kutoa urahisi kwa wateja wa Vodacom kupata huduma bora.
Amesema  hilo ni duka la kumi na moja katika mkoa wa Dar es salaam mbali na  maduka madogo madogo yaliyozagaa kila kona yanaitwa Vodacom Duka ambayo  kwa pamoja yanatenegza mtandao mpana wa kuhudumia wateja na jamii kwa  ujumla kwa ukaribu zaidi katika kiwango cha ubora wa hali ya juu
“Hili  ni duka letu la kumi na moja katika mkoa wa Dar es salaam ni azma ya  Vodacom kuona kwamba mteja anahudumiwa na kufikiwa na huduma kwa uharaka  na urahisi zaidi ili waweze kujiskia ufaghari kuwa miongoni mwa familia  kubwa ya wateja zaidi ya milioni kumi na moja”Alisema Tzamburakis.
Amesema  ukuaji wa Vodacom katika soko la mawasiliano ya simu za mkononi  unachagizwa pamoja na mambo mengine na udhati wa kampuni hiyo katika  kuwahudumia wateja wake kwa kiwango cha ubora unaoendana na hadhi ya  kampuni bila kujali aina ya mteja anaehudumiwa kwa kuzingatia kwamba  kila mteja wa Vodacom ana haki sawa ya kupata huduma bora zitakomfanya  mwisho wa siku kutabasamu.
“Tumethubutu  kuleta duka hili katika eneo hili la biashara tukiamini litawahudumia  vema wateja wetu wa maaeneo ya Buguruni,Gongolamboto, Chang’ombe, na  maeneo mengine ya Wilaya ya Temeka na Ilala hivyo ni imani yetu kwamba  kwa hatua hii wataendelea kujivunia kuwa wateja wa kampuni ya  Vodacom”Alisema Tzamburakis
Tzamburakis  amesema Amesema duka hilo litatoa huduama zote kwa wateja ikiwemo  huduima za M-PESA, usajili, manunuzi ya muda wa hewani na bidhaa  mbalimbali za Vodacom ikiwemo WEB BOX simu za mkononi na Moderm na  kwamba ni azma ya Vodacom kuimarisha mtandao wa maduka yake nchi nzima  ili kuendana na kasi ya ukuaji kibiashara na mahitaji ya wateja sokoni.

FAINALI ZA MASHINDANO YA MITUMBWI ZANOGA


Washiriki wa shindano la Mitumbwi Balimi Extra Lager wakiwa katika usahili wakijiandaa kuanza mashindano Mwaloni Jijini Mwanza mwishoni mwa wiki.

Washiriki wa shindano la Mitumbwi Balimi Extra Lager wakiwa tayari kuondoka wakisubili filimbi kupulizwa

Washiriki wa shindano la Mitumbwi Balimi Extra Lager wakiondoka baada ya filimbi kupulizwa.

Washiriki wa shindano la Mitumbwi Balimi Extra Lager wakiwa katikati ya maji wakati a shindano hilo .

Wakazi wa Jijini Mwanza wakishuhudia mashindano ya Mitumbi ya Balimi Extra Lager Mwaloni Jijini Mwanza mwishoni mwa wiki

Mkuu Wa Mkoa Wa Rukwa Mhe. Eng. Stella Martin Manyanya (MB) Ameliomba Shirika la Tanesco Wasikate Umeme Mkoa Rukwa Kipindi Hiki Cha Maandalizi Ya Sensa Ya Watu


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Eng. Stella Manyanya (MB) kulia na Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Eng. Stella Martin Manyanya (MB) ameliomba shirika la Uzalishaji na Usambazaji Umeme nchini (TANESCO) kuhakikisha upatikanaji wa Umeme unakuwa wa uhakika Mkoani Rukwa katika kipindi hiki cha maandalizi ya Sensa ya watu na makazi itakayokamilika mwezi februari mwaka 2012.
Sensa ya Watu na Makazi inategemewa kufanyika mwakani (2012) ambapo zoezi hilo litafanyika nchi nzima. Lengo kuu la Sensa ni kuweza kutambua idadi ya watu pamoja na kuainisha mahitaji yao muhimu yakiwemo huduma za jamii na kuweza kuyafanyia kazi kwa kuyaingiza katika mipango ya kitaifa na bajeti kwa ujumla.
Akizungumza na Timu ya sensa ya Mkoa wa Rukwa ambayo pia yeye ni mwenyekiti wake na ile ya sensa kutoka Tume ya Taifa ya Takwimu ofisini kwake akipokea taarifa na mkakati wa maandalizi ya zoezi hilo alisema kuwa ataiandikia TANESCO barua kuwafahamisha juu ya zoezi hilo na kuwaomba wajitahidi kuhakikisha kuwa umeme unakuwepo mkoani Rukwa kwa kipindi chote hicho cha maandalizi kuhakikisha ufanisi cha zoezi hilo ambalo linakwenda na muda.
Mkuu huyo wa Mkoa aliendelea kusema kuwa ni lazima tufikie azma ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ya kuendelea kutambua makazi ya wananchi wote wa Tanzania kupitia Sensa ya mwaka 2012 ili nchi iweze kuwa na mipango endelevu.
Zoezi hilo la maandalizi linahusisha utengaji wa maeneo rasmi kwa ajili ya kuhesabia zikiwemo kaya pamoja na maeneo muhimu yenye huduma za kijamii. Kwa kuanzia Timu hiyo inayoongozwa na Bwana Mugambi kutoka Tume ya Taifa ya Takwimu imejipanga kuanza na maeneo magumu ambayo ni tarafa za Mtowisa na Kipeta zilizopo katika Wialaya ya Sumbawanga.
Kwa upande mwingine Mkuu huyo wa Mkoa aliitaka Timu hiyo ya Sensa kwenda mbali zaidi katika zoezi hilo kwa kutaka kujua ni sababu zipi zinazopelekea wananchi kutotumia vituo maalum vya biashara vilivyojengwa na Serikali kwa gharama kubwa na badala yake kuendelea kufanya biashara zao katika maeneo yasiyo rasmi (mitaani) na kwamba pengine wanaweza kuja na majibu yatakayoweza kuondoa hali hiyo.
Kwa upande wake Katibu wa tume ya Sensa Mkoa wa Rukwa ambaye pia ni Katibu Tawala Mkoa huo Alhaj Salum Mohammed Chima amesema changamoto kubwa inayokabili Sekretarieti za Mikoa nchini ni ushirikishwaji hafifu katika upangaji wa bajeti za kitaifa hali inayopelekea Mikoa kupewa bajeti ndogo ukilinganisha na ile inayopelekwa wizarani.
Sensa ya mwisho iliyofanyika Agosti 2002 wakazi wa mkoa wa Rukwa walikuwa 1, 136, 354 na ambapo mpaka kufikia mwaka 2010 Mkoa huo unakiksiwa kuwa na wakazi 1, 503, 183 ambao ni ongezeko la asilimia 3.6% kwa mwaka.
Hamza Temba
Afisa Habari Mkoa
RUKWA

MADA MAUGO AMTWANGA SELEMANI SAIDI KWA KO RAUNDI YA TATU


Bondia Mada Maugo (kulia) akimsukumia konde zito mpinzani wake Seleman Said, wakati wa pambano la la raundi 8, lililofanyika jana usiku kwenye Ukumbi wa Mzalendo Pub, ambapo katika pambano hilo Mada alishinda kwa KO katika raundi ya tatu ya mchezo. Picha na Rajab Mhamila
Mwamuzi wa mchezo huo, akimhesabia bondia, Selemani Saidi, Baada ya kupokea kichapo na kuanguka katika raundi ya tatu, ambapo alishindwa kuinguka na mchezo huo kumalizika katika raundi hiyo.

RAIS JAKAYA KIKWETE AWAAPISHA MABALOZI WAPYA IKULU DAR LEO


Go to full article

Rais Jakaya Kikwete, akimwapisha, Phillip  Marmo, kuwa Balozi wa China, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha mabalozi wapya iliyofanyika leo mchana Desemba 19, Ikulu Dar es Salaam. Mabalozi wapya waliofika Ikulu Dar es Salaam leo kwa ajili ya kuapishwa na Rais Jakaya Kikwete, wakisubiri kuapishwa. Rais Jakaya Kikwete, akimwapisha, Dkt. Batilda Buriani, kuwa Balozi wa Kenya, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha mabalozi wapya iliyofanyika leo mchana Desemba 19, Ikulu Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete, akimwapisha, Dkt. Deodorus Kamala, kuwa Balozi wa Ubelgiji, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha mabalozi wapya iliyofanyika leo mchana Desemba 19, Ikulu Dar es Salaam.

Rais Jakaya Kikwete, akimwapisha, Ally A. Saleh, kuwa Balozi wa Oman, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha mabalozi wapya iliyofanyika leo mchana Desemba 19, Ikulu Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete, akimwapisha, Shamim Nyanduga, kuwa Balozi wa Msumbiji, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha mabalozi wapya iliyofanyika leo mchana Desemba 19, Ikulu Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (kushoto), Waziri  Mkuu, Mizengo Pinda (kulia) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, wakizungumza jambo, baada ya kumalizika kwa hafla fupi ya kuwaapisha mabalozi wapya iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam leo, Desemba 19. Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri  Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Maalim, wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wapya baada ya kuapishwa rasmi leo Ikulu Dar es Salaam.
Samim Nyanduga, akipongezwa na Mumewe, baada ya kuapishwa rasmi kuwa Balozi wa Msumbiji, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam leo. Nyuma yao ni wanafamilia wa Familia hiyo.

 

Picha Zote na Muhidin Sufiani-OMR